Рет қаралды 53
Darsa ilifanyika Swafar 21, 1446 H Jumapili Agosti 25, 2024
Akili ya mtoto itakapochanganyikiwa, na kupelekea hisia , fikia na mawazo kuvurugika na kuchafuka, na kusasabisha vitendo, miamala,tabia kufikia kuwa kinyume na maadili ya kawaida basi hali hii huweza kufikia kuleta magonjwa ya AKILI kwa mtoto.
Ugonjwa wa akili ni kitu ambacho humpelekea mtoto kuwa na hisia, mawazo, fikra, muono, na wakati mwengine hata matendo yake hufikia kuwa tofauti na yale anayotarajiwa kuwa nayo mtoto wa kawaida.
Ugonjwa wa akili hupelekea mtoto kufikia kushindwa kukabiliana na maisha ya kawaida wachilia mbali changamoto za kimaisha.