Рет қаралды 39
Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA kimewaagiza mawakili wa chama hicho chini ya Makamu Mwenyekiti wa Chadema Tundu Lissu kumfungulia mashtaka kamishina oparesheni na mafunzo ya polisi Awadh Juma Haji na Msajili msaidizi wa vyama vya siasa Sisty Nyahoza.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam, Mwenyekiti wa Chadema Taifa Freeman Mbowe amesema ni wakati wa chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania kuwawajibisha kiongozi.