Рет қаралды 5,162
Dainess Shao, mama mzazi wa Mkaguzi wa ndani wa Halmashauri ya wilaya ya Korogwe, mkoani Tanga, Jonais Shao(46) aliyefariki yeye na mwanaye Deidan Shao(7) kwa kuchomwa moto, ameeleza namna alivyokuwa akimsubiri mwanaye huyo siku ya alhamis aje amzike baba yake mdogo, ambaye alifariki dunia siku za hivi karibuni.
Mama huyo akisimulia kwa uchungu, amesema mwanaye huyo alikuwa ni mtoto wake wa kwanza na alikuwa ndio tegemeo lake kubwa baada ya baba yake mzazi, Edward Shao kufariki dunia miaka michache iliyopita.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Septemba 23, mwaka huu na Kamanda wa polisi mkoa wa Tanga, Almachius Mchunguzi ni kwamba miili ya watu hao ilikutwa imechomwa moto na watu wasiojulikana, usiku wa saa tatu, Septemba 23, mwaka huu eneo la msitu wa Hifadhi ya Korogwe Fuel, uliopo kijiji cha Sindeni wilayani Handeni, mkoa wa Tanga.
Kamanda Muchunguzi alisema jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi kuwatafuta wa husika wa tukio hilo.
Video na Ombeni Daniel