Рет қаралды 1,700
Ikiwa saa chache zimebakia kabla ya kuanza operesheni ya bomoabomoa, taharuki imetanda kwa baadhi ya wananchi wa Mtaa wa Malela Kata ya Toangoma Wilaya ya Temeke, wanaodaiwa kuvamia na kujenga makazi katika eneo la Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF)
Tukio hilo, litakaloacha simanzi kwa takribani kaya 600 zliizongia ndani ya eneo hilo, linatarajia kuanza kesho asubuhi baada ya kuahirishwa leo kutokana na maandalizi hafifu.
Hata hivyo,wavamizi hao licha ya kukiri kosa hilo, lawama zao wameelekeza kwa madalali wanaodai waliwalaghai kwa kuwauzia viwanja hivyo kwa gharama kubwa huku wakijua wazi ni mali ya NSSF.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Mwananchi baada ya kutembelea eneo hilo, wameiomba Serikali kuingilia kati sakata hilo, huku wakieleza viwanja hivyo waliuziwa kuanzia Sh 10 milioni na kuendelea na madalali hao wakiwa pamoja na viongozi wa mtaa huo.
Akizungumza na Mwananchi akiwa eneo hilo,Meneja Miliki wa (Nssf),Geofrey Timoth amesema maeneo hayo ni mali yao na wamekuwa wakilipia kodi kila mwaka na wavamizi hao wanajua.
(Imeandaliwa na mwandishi wetu)
#samiasuluhuhassan #simbasc #yangasc #mashabiki #nbcpremeireleague #cafchampionsleague #cafconfiderationcup #ikulumawasiliano #entertainment #music #news #yangasc #simbasc #cafchampionsleague #mayele #highlights #cafconfiderationcup #riversunited #mashabiki #yangaleo #yanga #timuyawananchi #daimambelenyumamwiko #entertainment #music #news #magoliyasimba #magoliyayanga #magoliyote #magoliyamayele #mayele #aziziki #manara #manaraleo #ikulumawasiliano #magufuli #kikwete #mayele #singidabigstars #magoliyamayele #magoliyasimba #magoliyayanga #highlights #azamsportsfederationcup #chama #Shot #mamelodisundowns #alahlytv #alahlysc #miraj