Рет қаралды 13,470
Mwanamke mmoja ameshtakiwa kwa njama ya kutaka kumuua mumewe mnamo tarehe 17 mwezi huu katika eneo la Zimmerman hapa jijini. Faith Wairimu Maina anadaiwa kuwalipa maafisa wa polisi kutoka idara ya flying squad sh alfu 40 ili wajifanye majambazi na kuumuua mumewe John Muthee Guama. Polisi hao walimshika mateka John na baadaye kumfichulia siri kuhusu njama ya kuuwawa kwake.