Рет қаралды 5,323
Meli kubwa zaidi iliyobeba watalii zaidi ya 2,340 kutoka Canada imewasili alfajiri ya leo Jumanne Januari 16, 2024 katika bandari ya Dar es Salaam.
Meli hiyo ya kitalii inayoitwa Norwegian Cruise Line Dawn yenye urefu wa mita 294 imetajwa kuwa kubwa zaidi kuwasili katika bandari zote nchini tangu kuanzishwa kwake. Norwegian Cruise Line Dawn ilianza kufanya kazi mwaka 2002 ikiwa na thamani ya zaidi ya Sh 1trilioni.
Norwegian Cruise Line Dawn pia ina kimo cha mita 59, ikienda kwa kasi ya kilomita 46 kwa saa na ina wafanyakazi zaidi ya 1000.
Mkurugenzi wa bandari ya Dar es Salaam, Mrisho Mrisho amewaambia wanahabari leo kuwa meli ya Norwegian Cruise Line Dawn hadi inafika Tanzania imepitia katika bandari tofauti ikiwemo Mombasa Kenya, akisema ina uwezo kubeba abiria 4700, lakini waliowasili ni watalii 2,210.