Рет қаралды 12,627
Mamia ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Jomo Kenyatta wameandamana hii leo kudai haki kufuatia kifo tatanishi cha mwenzao denzel omondi ambaye mwili wake ulipatikana ndani ya mgodi huko Juja. Wanafunzi hao ambao walifunga barabara kuu ya thika wamekataa matokeo ya uchunguzi wa maiti wakishikilia kuwa mwenzao aliuawa kwa kuhusika katika maandamano dhidi ya serikali