Рет қаралды 8
Katika kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja shirika la umeme Tanesco mkoa wa Simiyu limekiri kuwa changamoto ya umeme ni kubwa mkoani hapa hali inayochangizwa na kutokuwa na kituo cha kupozea umeme.
Akizungumza wakati wa zoezi la kuwatembelea wateja wanaopata changamoto za umeme leo Octoba 6,2022 meneja wa shirika hilo Alistidia Clemence amesema changamoto wanazichukulia kama fursa za kuweza kuboresha huduma.
Huduma ya kuwafikia wateja majumbani imeambatana na kutoa zawadi wateja wakubwa ambapo baadhi ya wateja wametinukiwa vyeti vya shukrani pamoja na kupewa zawadi ikiwamo kukata keki.
Kwa upande wa huduma ya nikonect mkoa wa Simiyu jumla ya wateja 1340 wameunganishiwa umeme kupitia huduma hiyo, hivyo kufanya jumla ya wateja wa tanesco kufikia 3945 walio katika vijiji 269 na vijiji 201 pekee vimesalia kupata huduma ya umeme.
Mwisho.