Рет қаралды 422
Balaa la MAKONDA Arusha, Maelfu ya Wananchi wafurika kupata matibabu Bure
WAZEE, WAJAWAZITO NA WATOTO KUPEWA KIPAUMBELE KAMBI YA MADAKTARI BINGWA ARUSHA - RC MAKONDA
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Makonda , ameweka wazi kuwa kulingana na hali za wazee, wajawazito na watoto hivyo kuanzia siku ya ijumaa tarehe 28 Juni, 2024 kupitia kambi ya madaktari bingwa na wabobezi wataanza kupewa kipaumbele zaidi kwa kuwekewa utaratibu wao kuweza kuwarahishia katika kupata huduma hizo za matibabu.
Akizungumza na maelfu ya wananchi waliojitokeza kwa wingi katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid , RC Makonda amesema lengo la Kambi hiyo ni kuendelea kuwafuta machozi wanandchi wanyonge waliokuwa wakipambania afya zao.