Рет қаралды 388
CCM YAPONGEZA HOTUBA ya RAIS SAMIA KUKEMEA UTEKAJI na MAUAJI - AMOS MAKALA - "WANAPOTOSHA"....
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimempongeza Rais DK Samia Suluhu Hassan kwa hotuba yake aliyoitoa Kilimanjaro ya kukemea vitendo vya utekaji na mauaji huku akiliagiza jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa kina kubaini wale wanao husika na vitendo hivyo huku kikilaani vitendo hivyo vya upotoshaji wa hotuba hiyo vinavyofanywa na wapinzani hususan Chadema.
Pia, alisema CCM imejipanga vizuri kushinda kwa kishindo Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kutokana na maandalizi makubwa waliyoyafanya na kazi nzuri iliyofanywa na Rais Dk.Samia ya kutekeleza miradi mikubwa na kupeleka fedha nyingi vijijini za utekelezaji miradi ya maendeleo.
Pongezi hizo zimetolewa jana na Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla alipokuwa akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya siasa Mkoa wa Dar es Salaam.
"Mheshimiwa Rais alitoa kauli ile, akiwa Rais, kiongozi mkuu wa nchi na Amiri jeshi Mkuu, alitoa kauli Ile lakn watu wenye Nia mbaya wamekuwa mitandao na wengine katika vikao vyao wamekuwa wakipotosha na kulipa maana nyingine...