Рет қаралды 37,445
Yoshua 24:14-15
Basi sasa mcheni BWANA, mkamtumikie kwa unyofu wa moyo na kwa kweli; na kuiweka mbali miungu ambayo baba zenu waliitumikia ng’ambo ya Mto, na huko Misri; mkamtumikie yeye BWANA.
Nanyi kama mkiona ni vibaya kumtumikia BWANA, chagueni hivi leo mtakayemtumikia; kwamba ni miungu ile ambayo baba zenu waliitumikia ng’ambo ya Mto, au kwamba ni miungu ya wale Waamori ambao mnakaa katika nchi yao; lakini mimi na nyumba yangu tutamtumikia BWANA.
Lyrics
Ee Israeli Leo ninataka ukumbuke
Nilipokutoa hadi nilipokufikisha
Nilisikia kilio chako ulipolia
Utumwani Misri penye mateso na huzuni
Ndipo niliponyosha mkono
kukuokoa hata kukusamehe
Lakini ulipofanikiwa ukageukia miungu mingine
Oh Leo hii nataka tufanye agano
Kama ni rehema nimeshazitoa
Je ni Nini sijakifanya?
Chagueni hivi leo mtakayemtumikia maishani mwenu
Je ni Mungu aliyewatoa utumwani?
Ooh
kumbukeni alivyowavusha katika bahari na kuwapa chakula.
Mimi na nyumba yangu tumemchagua,
nakushauri nawe umchague.
Ee mwanadamu Bwana Mungu leo anasema
Je Mimi si Mungu ninayekutakia mema?
Ni Mara ngapi nimejaribu kuwakusanya
Kama kuku akusanyavyo vifaranga vyake
Tambua nimeshafanya yote
Kuokoa nafsi yako 'sipotee
Hata kumtoa Yesu afe
Ili kulipa deni la kifo chako
Oh! Na zaidi (Oh na zaidi)
Nimekupa ahadi Tamu
Ahadi ile ya uzima milele
Siku Yesu atakapokuja.
Basi chagueni
Chagueni hivi leo mtakayemtumikia maishani mwenu
Je ni Mungu aliyewatoa utumwani?
Ooh
kumbukeni alivyowavusha katika bahari na kuwapa chakula.
Mimi na nyumba yangu tumemchagua,
nakushauri nawe umchague.
Artist: Dodoma Adventist Chorus
Song Title: Chagueni
Audio Mixing and mastering: BJ Brand
Video: RJ Studio (Mr RJ)
Email: dodomaadventistchorus21@gmail.com
CONTACTS
+255 746 698 570
+255 622 309 142
You can also find us on:
Audiomack: audiomack.com/...
Instagram
/ dodomaadventistchorus
and all digital platform.