Рет қаралды 4,510
Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania - TFS iko kwenye kampeni ya kuhakikisha kwamba Sekta ya Maliasili inazidi kuimarika ili kuyafanya mazao yatokanayo na maliasili hususan misitu na nyuki yanaendelea kuchangia katika ukuaji wa uchumi, kuwaongezea wananchi kipato na kuongeza fursa za ajira. Aidha, ili kuwajengea uwezo wadau wake kuzifahamu mbinu bora za uzalishaji wa mazao ya nyuki na pia masoko ya asali na nta ya ndani na nje ya nchi Wakala imeandaa Maonesho ya Asali na Bidhaa za Mianzi yatakayofanyika mwezi Mei, 2018 katika tarehe itakayotajwa siku za usoni. Wakala inatoa wito kwa Watanzania kufuga nyuki kwa wingi ili kukuza uchumi kwa kutumia fursa ya upatikanaji asali na nta kutokana na uwepo wa soko la uhakika la ndani na nje ya nchi badala ya kukata miti ovyo kwa shughuli za uchomaji mkaa.