Рет қаралды 10,455
Familia ya daktari mwanagenzi Laban Lang’at aliyeuwawa na watu wasiojulikana na mwili wake kupatikana katika hospitali ya Nakuru level 5 imelalamikia hali ya uchunguzi kuendeshwa kwa mwendo wa kinyonga. Familia hiyo iliyompumzisha mpendwa wao katika kijiji cha Chematich, kaunti ya Trans-Nzoia inaitaka idara ya polisi kuharakisha uchunguzi na kuwanasa washukiwa. Collins shitiabayi na taarifa hiyo.