Рет қаралды 7,834
Licha ya vitisho vya waziri wa usalama Kithure Kindiki kuhusu utepetevu wa maafisa wa idara ya uhamiaji, maelfu ya wananchi bado wanahangaika kupata paspoti zao. Baadhi ya watu wanalazimika kwenda kila siku katika jumba la nyayo kutafuta hati za usafiri huku baadhi wakisema wamesubiri mwaka mzima. Ben kirui alizungumza na baadhi ya wakenya ambao wamekosa nafasi za kazi kwa kutopata paspoti kwa wakati unaofaa.