Рет қаралды 1,233
Tume ya Kudhibiti Ukimwi (Tacaids) imesema maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi (VVU) yamepungua kutoka watu 110,000 mwaka 2016/17 hadi kufikia 54,000 mwaka 2020/2021.
Hayo yamesema Mkurugenzi Mtendaji wa Tacaids, Dk Leonard Maboko, Jumanne Novemba 14,2022 wakati akizungumzia maadhimisho ya siku ya Ukimwi yanayofanyika Desemba Mosi kila mwaka.
Dk Maboko alisema idadi ya vifo pia imepungua kutoka vifo vinavyotokana na ugonjwa wa Ukimwi 64,000 mwaka 2016/17 hadi kufikia vifo 29,000 mwaka 2020/21.