Рет қаралды 82
Katika kuongeza zao la samaki nchini wilaya ya kishapu mkoani Shinyanga imeanza zoezi la upandikizaji wa samaki (12,0000) aina ya sato, katika bwawa la mhumbu kata ya Somgwa wilayani humo
Kaimu Mkurugenzi halimashauri ya wilaya ya kishapu Sabiusi Chaula amesema kupitia bajeti ya mwaka 2022-2023 wameweza kununua vifaranga vya samaki elfu 12 ili kuwawezezesha wavuvi kuendelea kujipatia kipato.
Akieleza malengo ya kufanya upandikizaji wa samaki katika bwawa hilo Afisa uvuvi wilaya ya kishapu Moses Zacharia amesema nikuongeza wingo wa upatikanaji wa zao la samaki,huku Katibu tawala halimashauri ya wilaya ya kishapu shadrack Kengese amewataka viongozi wa vijiji, kata na jumuia za watumia maji kulinda vyanzo vya bwawa hilo.
Nao wakazi wa wilaya ya kishapu wameahidi kulinda na kulitunza bwawa hilo ili liweze kuwanufaisha huku wakiiomba serikali iweze kuwapatia ushirikiano kuhakikisha vifaranga hao wa samaki wanakua ili wameze kuwapatia kitoweo na kipato.