Рет қаралды 4,300
Afisa habari wa Simba SC Ahmed Ally,amesema wanasimba msiwe wanyonge kisa Chama kuondoka Simba SC kwani maisha yajayo bila yeye yanaweza kuwa mazuri zaidi hivyo mzidi kuipenda Simba kama mnavyoipenda siku zote
"Wale mliyokuwa mnampenda Chama,Chama ameshaondoka ndani ya Simba SC lakini wale waliyokuwa wanaipenda Simba,Simba bado ipo
Maana yake ni kwamba tunapaswa kuendelea kuishi na misingi yetu ileile tukiyokuwa tukiishi nayo zamani ya kuipenda na kuisapoti Simba yetu
Simba ilikuwepo na itakuwepo ni sisi wana Simba sasa kukubali maisha mapya na inawezekana yakawa ndio maisha bora zaidi kuliko yale ambayo tungetamani kuendelea nayo