Bwana Leonard Kushoka: Binafsi nakupongeza sana wewe binafsi na kampuni yako ya Kuja na Kushoka kwa ubunifu wa mashine za kutengenezea mkaa mbadala. Yaani mkaa ambao unatengenezwa kwa takataka za shambani na viwanda vya mbao, ambao unawaka vizuri sana (niliununua na kuutumia kwa kuchomea nyama hapo kwangu, hauzimi!), bei nafuu, na muhimu zaidi unasaidia kulinda mazingira kwa kuepusha kufyekwa kwa miti. Lakini zaidi ya hapo umebuni majiko banifu (improved cook stoves) kwa majumbani na kwenye taasisi. Hali kadhalika mnatengeneza mashine nyingine nyingi za ujasiriamali. Hongera sana👏🏾🙏🏾 Njia ni ndefu na changamoto hazikosi, lakini bidii ba ustahimilivu wenu utalipa tu, hasa kwa vile sasa wanasiasa wameanza kuwaunga mkono!