Рет қаралды 9,036
Ni kawaida kwa watoto wengi kuwa na ndoto ya kuwa daktari ama wazazi kupendelea wana wao kusomea taalamu hiyo. Lakini kwa Daktari Mwanabule haikuwa kwenye fikra zake kwamba angewahi kuwa daktari tena wa kutajika.na si hayo tu, dkt Bule kama anavyojulikana ni mwanamke wa kwanza daktari wa upasuaji jijini mombasa. Je safari yake ya kufuzu kwenye taalamu hiyo imekuwaje? nilipata fursa ya kutangamana naye huko likoni na kuandaa simulizi ifuatayo kwenye makala yetu ya mwanamke bomba.