Рет қаралды 6,228
Mzozo umeendelea kutokota kuhusu hatma ya atakapozikwa kijana wa miaka 12 aliyepigwa risasi wakati wa maandamano eneo la Rongai kaunti ya Kajiado. Utata kati ya baba na mamake mtoto Kennedy Onyango sasa ukisababisha kusitishwa kwa mazishi yake kaunti ya Homa Bay. Licha ya mama kuandaa mazishi ya mwanawe, babake mtoto alielekea mahakamani kutaka apewe idhini ya kumzika kijana wake.