Рет қаралды 129,996
Kwa miaka miwili alikuwa akiandika katika mchanga, manaake alikuwa hana kitabu wala kalamu. Na wengi hawakubaini kwamba kijana huyo kutoka eneo la Gatuyaini, Othaya ambaye alifanikiwa kupelekwa shule kwa sababu alikuwa kitinda mimba katika familia yake- atatawala Kenya kwa miaka kumi. Shajara ya rais Kibaki ina mengi, lakini sio mengi katika ujana wake wanayafahamu wakenya. Na ili kufahamu mengi zaidi kuhusu huyu Emilio Mwai Kibaki, Carol Nderi alizuru eneo la Gatuyaini na kukutana na ndugu zake rais Mwai Kibaki,dadake Esther Waitherero na kakake Benard Ndiritu Kibaki
Watch KTN Streaming LIVE from Kenya 24/7 on www.ktnkenya.tv