Рет қаралды 3,178
Leo tunazungumzia Msitu wa asili wa Nyumbanitu uko Njombe unajumuisha msitu pamoja na mapango. Msitu wa asili wa nyumbanitu wenye ukubwa wa hekta moja na nusu unatunzwa kimila na ni moja ya kivutio kikubwa sana mkoani Njombe.
Katika msitu wa nyumbanitu uliobeba maajabu ya aina yake hutumika kwa ibada za asili na unadaiwa kuwa na ngombe na kondoo weusi ambao wana historia ya aina yake yapo mapango ambayo yalitumiwa na wabena kujificha wakati wa vita.
Unapoanza kuingia tu katika msitu wa nyumbanitu (Nyumba nyeusi) ukibahatika basi unaweza kutana kuku weusi ambao hawaliwi na wala huwezi kuona wanataga wapi au wanalala wapi wakati mwingine hutembea makundi wakiwa watano au mmoja au wawili na tulipofika hapa tulipokelewa na mmoja wa kuku hao wa maajabu.
Sharti moja wapo la kuingia katika msitu wa nyumbanitu (Nyumba Nyeusi) ni lazima kuvua viatu na kutembea peku kwakufuata mstari lakini pia kuvaa kofia na vilemba hairuhusiwi uingiapo ndani ya msitu huu uliobeba historia ya kipekee.
Inaelezwa kwamna Mnamo mwaka 1948 hadi 1958 kampuji yabkizungu iliyopanda miti ya kisasa ndipo ilipoingia ambapo walikaribishwa na chifu wa wabena Joseph mbeyela, ambapo aliwataka kutoharibu uoto wa asili na miti ya asili katika eneo hilo lakini walikaidi na kufyeka baadhi ya eneo la msitu kwa kuwa hawakuamini mila zetu ndipo wakakumbana na maajabu.
Inaelezwa kuwa kila walipokata miti ilikuwa haidondoki inabaki imesimama kama kawaida. Na hapa kiongozi wa kimila wanaosimamia msitu huo ana eleza zaidi.
Lakini pia katika msitu huu yapo mapango makubwa sana ambayo yanadaiwa kutumiwa na watu wakati wa vita ikiwamo makazi ya ngombe wa ajabu waliokuwa wakizuka na kupita kuelekea msitu wa nyumbanitu kama anavyoeleza hapa mzee wa kimila Alex wangameli Msigwa.
Dada mujifadhi pamoja na Isaya mwaka jana bado tunachanja mbuga kuiangazia kusini utalii na tamaduni zetu endelea kuambatana nasi
Dada mujifadhi Sophia kessy ameweka kambi maendeo hayo ambapo leo anatupa undani huo kutokea njombe.