Рет қаралды 31
Wizara ya Maliasili na Utalii imewataka wadau wa sekta ya Utalii nchini kujiandaa kupokea watalii wengi katika kipindi kifupi kijacho kufuatia mafanikio yanayotarajiwa kwenye kampeni maalum iliyoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ya kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini kupitia kipindi maalumu cha Royal Tour
Akizungumza wakati wa mahafali ya 19 ya Chuo cha Taifa cha Utalii NCT jijini Dar es Salaam, Naibu waziri wa Wizara hiyo Mary Masanja amesema kupitia kampeni ya kipindi cha Royal Tour kitakachorushwa nchini Marekani, Rais amejenga ushawishi mkubwa kwa watalii kwamba Tanzania ni eneo salama lakutembelea.
Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa Chuo hicho Dkt. Shoko Mlozi ameishukuru serikali kwa maboresho yaliyofanyika kwenye kampasi za Chuo hicho nakuongeza ufanidi katika utoaji wa elimu kwa watoto wa Kitanzania.
Zaidi wa wanafunzi mia tano wamehitimu nakutunukiwa vyeti katika kozi mbalimbali katika Chuo hicho.