Рет қаралды 1,076
Moja ya kipengele moto zaidi katika Tamasha la #Back2sua October 2023 ambapo washindani sita (6) Mapengo Boy (From Sekei), Toxic Man (From Sanawari), Dizzla (kutoka Sakina), Mashineboy Kevi (kutoka Kijenge), RMC (kutoka Kijenge) na Sobibo Khan (kutoka Morombo). waliazimia kuingia vitani.
Baada ya raundi kadhaa za mchujo, raundi ya mwisho ilikuwa baina ya RMC na Sobibo Khan. Wote wawili walionyesha umahiri na kujiamini katika Sanaa ya mitindo huru. Baada ya mtanange mzito mshindi aliibuka kuwa ni Sobibo Khan. Waamuzi wa vita hii walikuwa umati wa #Back2sua.
Kwa heshima ya Utamaduni wa Hip Hop, msanii maarufu wa hip-hop Mo Plus(wa Ukoo) alimpa zawadi Sobibo Khan kuwa Mfalme mpya wa Freestyle 2023.
Zawadi ya pambano la freestyle la S.U.A mwaka 2023 lilikuwa TZS.200,000/- na zawadi mbalimbali kutoka kwa Okoa Mtaa Foundation, kama fulana na vibandiko.