Рет қаралды 70
Taasisi ya uhandisi na usanifu mitambo Tanzania (TEMDO )imebuni teknolojia mbalimbali ikiwemo majokofu ya kuhifadhia miili,vitanda vya kujifungulia wakinamama ,pamoja na viteketeza taka katika hospitali, ambapo watanzania wametakiwa kuchangamkia fursa ya kununua teknolojia hizo zinazozalishwa hapa nchini badala ya kuagiza nje ya nchi.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi mkuu wa TEMDO, Injinia Prof. Frederick Kahimba wakati akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea kwa lengo la kujionea teknolojia mbalimbali zinazotengenezwa ikiwa ni sehemu ya mafunzo kwa vitendo kwa waandishi waliopatiwa elimu namna ya kuandika habari za Sayansi na teknolojia yaliyoandaliwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia Tanzania (COSTECH).