Рет қаралды 244,021
Makamu Mwenyekiti wa Chadema Tundu Lisu amefika kwenye ofisi ya Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma RPC Martin otieno akitaka kuliangalia gari lake ambalo anadai alishambuliwa akiwa kwenye gari hilo.
Lissu amefika leo Alhamisi, Februari 9, 2023, huku akisema kuwa alikuwa amewasiliana na RPC kwaajili ya kwenda kuliona gari lake hilo ambalo hata hiivyo bado hajafanikiwa kuliona akielekezwa kurudi wakati mwingine kutokana na RPC kuwa kwenye shughuli nyingine.