Рет қаралды 1,341
Wakaazi wa vijiji vinnne katika wadi ya Muvau Kikumini kaunti ya Makueni wameitaka serikali ya kaunti hiyo kuingilia kati kuhakikisha changarawe zilizoziba bwawa eneo hilo zinaondolewa. Wakaazi wanasema bwawa hilo linategemewa kwa huduma za maji ya matumizi na mifugo kwa wakaazi zaidi ya elfu nne.