Рет қаралды 3,746
Tangu kupata uhuru hadi miaka ya 1990, Tanzania ilikuwa mstari wa mbele kupigania ukombozi wa nchi za Afrika hususan zile za Kusini mwa Afrika
kutoka katika utawala wa kikoloni sanjari na kupinga ubaguzi dhidi ya mwafrika. Katika kipindi hicho, Tanzania ilichangia rasilimali fedha, askari pamoja na ardhi yake kusaidia wapigania uhuru kutoka nchi nyingine za Afrika ikiwemo Angola, Namibia, Zimbabwe, Afrika Kusini na Msumbiji.
Imani ya waasisi wa nchi yetu wakati huo ilikuwa ni kwamba uhuru wa Tanzania hautakuwa kamili endapo nchi zinazotuzunguka zitakuwa hazijapata uhuru wa kujitawala zenyewe.