Рет қаралды 24,157
Mbunge wa Jimbo la Kwimba mkoani Mwanza, Shanif Mansoor (CCM) amewekeza zaidi ya shilingi bilioni moja katika shamba kubwa la kisasa la ufugaji wa kuku wa mayai wapatao elfu 35 katika eneo la Nyanguge wilayani Magu mkoani hapa.
Pamoja na kufunguka kuwa kwa sasa anauhaba wa mahindi kwa chakula zaidi ya tani elfu sitini, Mansoor ambaye ni Mkurugenzi wa shamba hilo liitwalo SMJ Poultry Eggm Farm amesema kuwepo kwa shamba hilo kumekuwa fursa kwa wakazi wa wilaya ya Magu kupata ajira licha ya kukabiliwa na changamoto ya uingizwaji wa mayai ya magendo toka nje ya nchi.