Рет қаралды 34
Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknologia Omary Kipanga amewataka viongozi wa Mkoa wa Simiyu, Pamoja na Wilaya ya Bariadi kusimamia kwa karibu mradi wa ujenzi wa Chuo cha ufundi Stadi (VETA) kwa kufuata kanuni na miongozo iliyowekwa na Wizara katika ujenzi wa Mradi huo.
Naibu Waziri huyo ametoa maagizo hayo leo, wakati wa ziara yake ya siku moja mkoani humo iliyolenga kukagua ujenzi wa chuo hicho ambacho kinajengwa katika kijiji cha Bunhamala halmashauri ya Mji wa Bariadi.
Kipanga amesema kuwa usimamizi wa karibu wa viongozi hao ni muhimu sana katika kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati katika ujenzi wake, lakini Wizara imetoa kanuni na taratibu zinazotumika kusimamia mradi huo ambazo lazima zifuatwe.