Рет қаралды 44,539
Kwa majina Naitwa hamadi juma ni mtoto wa kwanza katika familia ya watoto wawili Mimi na mdogo wangu wa kike aliyeitwa hasma juma nilibaatika kupata malezi ya wazazi wangu wawili kwa miaka 16 apo baba angu alipata kazi jijini dar es Salam kabla baba ajaondoka na kutuacha na mama tulikuwa na maisha ya kawaida tu sio ya shida Wala ya raha baba angu alikuwa ni fundi welding alikuwa akifanya kazi kwenye viwanda ndipo alipoipata kazi ya kwenda kujenga kiwanda jijin dar akuwa na jinsi akatuacha Mimi na mama angu pamoja na mdogo wangu hasma.Miezi mitatu ya mwanzo baba alikuwa tukiwasiliana nae na alikuwa anatuma maitaji yote ya nyumbani ila gafla simu ya baba aikuwa hewani na aikupatikana Tena tulifanya juhudi zote za kupata mawasiliano nae ila ilishindikana hata
ndungu zake kina baba wadogo na mashangazi jitihada ziligonga mwamba apo maisha yakaanza kuwa magumu nyumbani kwani majukumu ya kutulea yalibaki kwa mama amabae alikuwa ni mama wa nyumbani tu. Maisha yalibadilika Sana ilimbidi mama atafute vibarua kwenye mashamba ya watu ili aweze kutusomesha kutulisha na maitaji mengine.