Рет қаралды 91,468
December 30/2022 mtoto BENITHA aliongozana na wazazi wake pamoja na ndugu zake wengine kwenda kwenye mtoko wa familia maeneo ya Temboni Jijini Dar es salaam, Familia ikiwa yenye furaha huku wakimshukuru Mungu kwa kumaliza mwaka salama.
Katika hali isiyokuwa ya kawaida Mtoto Benitha alitoweka kwenye upeo wa macho ya wazazi jambo ambalo halikuwashtua wazazi sana kutokana na ukweli kwamba mtoto huyu tayari alikuwa ni mkubwa, miaka 13 anayejitambua na zaidi sana mtulivu wa akili.
Baada ya dakika kadhaa kama mzazi mwingine yeyote wakaona hii siyo hali ya kawaida, ndipo wakasimama kuangaza macho ili kuona mtoto yupo wapi
'MASKINI WEE!! Hawakujua kama ilikuwa ndiyo siku ya mwisho kumuona binti yao akiwa mzima wa afya.
Nini kilimpata mtoto Benitha?
Benitha alitumbukia kwenye Swimming pool bila ya mtu yeyote kubaini hali hiyo na kwa makadirio ya dakika 10 ndipo alipopata usaidizi ambao kimsingi haukuzaa matunda
Hapa Madaktari wanaelezea ni nini kilichofuata hadi umauti.