Рет қаралды 233
Leo nimepata fursa ya kuongea na Dk. Bingwa katika taaluma ya NYURO REDIOLOJI. Dr. Minja, ni mmoja wa madokta ambao wana shiriki sana katika kuikomboa nchi yetu nzuri ya Tanzania katika sekta ya AFYA haswa katika upande wa Radiology akishirikiana na hospitali kubwa kama Muhimbili katika kuboresha sayansi na teknolojia ya Radiology.
Dk. Minja pia amekuwa mstari wa mbele aki sapoti wana diaspora kwa kushiriki na kuongoza vikundi vinavyo wakilisha waTanzania waliopo nchi ya Marekani kama DICOTA.
Katika maongezi haya na Dk. Minja, ameweza kugusia kwa mbali jinsi gani technolojia ya Radioloji ina tumika katika kugundua magonjwa mbalimbali katika mwili wa binadamu ikiwapo magonjwa kama Kiarusi, shinikizo la damu kwenye ubongo n.k.
Dk. Minja pia ameweza kugusia vitu mbalimbali juu ya AFYA ya mwanaume haswa jinsi ya kuepuka magonjwa ambayo huweza kutokea kadri umri unavyoenda juu.
Kama una maswali basi usisite kuacha hapo chini kwenye comment!
Kama umeipenda hii video basi naomba uipe Dole gumba!
Pia naomba usisahau kushea link na video za Jiongeze Podcast katika social media zako na rafiki zako!
Kama bado hatuja fuatana basi fanya hivyo;
Ni follow IG @jiongezepodcast
Ni follow IG @MalkiaCynthia