Рет қаралды 2,626
#kenya imeshuhudia maandamano ya amani ambayo kwa kiwango kikubwa yameongozwa na vijana wa vuguvugu la #GenZ kupinga muswada wa sheria ya fedha ulionuia kuongeza kodi, maandamano ambayo yamegeuka kuwa ya machafuko. Hii ina maana gani kwa vuguguvugu hili na ni kipi kinachoweza kutokea kwa rais wa Kenya William #Ruto kufuatia maandamano haya? Josephat Charo anajadili mada hii na wachambuzi katika kipindi cha Maoni mbele ya meza ya duara.