Рет қаралды 150
Chuo Kikuu cha Iringa kupitia atamizi ya kulea na kuendeleza mawazo ya ubunifu na ujasiriamali, ijulikanayo kama Kiota Hub, kilitafuta suluhu itakayowasaidia wahitimu kujiajiri au kuajiriwa. Baada ya kufanya utafiti na kubaini kwamba wahitimu wengi hawaajiriki kutokana na kukosa sifa wanazozitaka waajiri, chuo hicho kilianzisha atamizi ya Kiota Hub
Mpaka sasa vijana 700 wamenufaika na mafunzo kutoka Kiota Hub, na kati yao wanawake 150 wamejiajiri wenyewe na 50 wameajiriwa kwenye Taasisi mbalimbali huku vijana 160 nao wakijiajiri na wengine 64 kuajiriwa