Рет қаралды 58,217
Takriban miaka tisa iliyopita, mamilioni ya watu kutoka Afrika Mashariki walifunga safari na kuelekea hadi kijiji cha Samunge nchini Tanzania kutafuta miujiza ya uponyaji wa magonjwa aina aina. Eneo la Loliondo likageuka na kuwa sehemu iliyosifika hasa miongoni mwa Wakenya. Dawa za uponyaji ambazo wakati huo zilionekana kuwa miujuzia zilikuwa zinatolewa na mhubiri aliyestaafu kwa jina Ambilikile Mwasapile maarufu Babu. Mwishoni mwa mwaka wa 2012 zaidi ya watu milioni 6 walizuru kijiji cha Samunge, sehemu anayoishi Babu hadi wa leo. Hii leo runinga ya Citizen imeandaa makala kuhusu matukio baada ya Loliondo ambapo wengi walifariki baadaye na wengine wakizungumzia masaibu yao. Huyu hapa Jamila Mohamed na makala ya Hekaya za Loliondo.
#HekayaZaLoliondo #TibaYaLoliondo