Рет қаралды 13,673
Nchini Tanzania kumeibuka mjadala unaohusu mustakabali wa utawala wa kisheria na haki za binaadamu, baada ya rais wa nchi hiyo, Samia Suluhu Hassan, kutoa kauli iliyotafsiriwa kwamba inatishia harakati za utetezi wa haki za binaadamu na mfumo mzima wa sheria. Rais Samia alitoa kauli hiyo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 27 wa jumuiya ya wanasheria wa Afrika Mashariki jijini Arusha Tanzania. #kurunzi