Рет қаралды 457,782
Anaona fahari kwa kuwa miongoni mwa wanajeshi wachache mno waliopata fursa ya kuwa dereva wa rais wa kwanza wa jamhuri ya Kenya Mzee Jomo Kenyatta. Japo ni miaka mingi baada ya kustaafu kwake, Martin Munuve Njema mwenye umri wa miaka 76 anakumbuka vyema hali ilivyokuwa alipokuwa dereva wa gari maalum alilotumia Mzee Kenyatta ilipowadia siku kuu ya kitaifa. Mwanahabari wetu Patrick Injendi alimtembelea nyumbani kwake mzee huyo huko Kithimani eneo la Mbooni kaunti ya Makueni ambako alimhoji zaidi kuhusu taarifa inayomhusu.