Рет қаралды 1,415
Baada ya kugonga vichwa vya habari kufuatia hatua ya wazee wa kijiji cha Mosora kufurusha familia za wale waliohusishwa na wizi, maafisa wa usalama hatimaye wameitikia wito wa kutuliza hali baada ya chifu na naibu wake kustaafu mwaka jana. Mkutano wa dharura uliandaliwa tena katika eneo hilo la Bobasi huko Kisii kujadili hatma ya waliofurushwa kijijini.