Рет қаралды 30
Kituo Cha Ukombozi, Chatekeleza Maelekezo ya Mhe. Ndumbaro, Kukarabati Handaki la Ukombozi Kongwa
Kituo Cha Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika, Kinaendelea na Utekelezaji wa Maelekezo ya Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo kuhusu Kukarabati haraka Handaki la Kihistoria lililotumiwa na Baba wa Taifa la Msumbiji Hayati Samora Machel kwa Lengo la kumuenzi na Kuhifadhi Historia hiyo.
Tayari Timu ya Wataalamu kutoka Maliasili na Utalii, Wilaya ya Kongwa na Kituo Cha Ukombozi wapo eneo Hilo wakihakikisha Ukarabati huo unazingatia kanuni za uhifadhi wa Malikale na majengo ya Kihistoria.
Urithi wa Ukombozi Fahari ya Afrika