Рет қаралды 63
Kituo cha Ukombozi kimetembelea eneo la Likuyu Sekamaganga lililopo Wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma, eneo ambalo lililopokea na kuhifadhi wapigania uhuru zaidi ya 1000 kutoka Msumbiji kuanzia mwaka 1979 wakati wa Vita vya Renamo na Frelimo vilivyoanza mara baada ya nchi hiyo kupata uhuru mwaka 1975.
Eneo hili liliwapokea wapigania uhuru wa Msumbiji na kuwapatia hifadhi katika vijiji 9 kikiwemo kijiji cha Mandela, Kambona, Kambarage, Kolimba, Sokoine, Samora na Mondlane vilivyopo katika Wilaya ya Namtumbo.
Aidha, Urithi unaopatikana katika eneo hili ni pamoja na Shule ya msingi Mandela, zahanati, Chuo cha Mafunzo ya Uhifadhi wa Maliasili kwa jamii (CBCT) na mashine ya kusagia nafaka.
Kituo kimetembelea eneo hili kwa lengo la kutambua urithi uliopo kwa ajili kuhifadhi, kutoa elimu kwa jamii na kutangaza utalii wa kiukombozi unaopatikana katika Wilaya ya Namtumbo.
Urithi wa Ukombozi, Fahari ya Afrika