Рет қаралды 42,545
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda amehoji kuhusu Utambulisho halisi wa Arusha na kutaka wana Arusha kujitafakari kuhusu kile kinachoutambulisha mkoa huo wa unaopatikana Kaskazini mwa Nchi.
Paul Christian Makonda ametoa kauli hiyo leo Aprili 13, 2024 alipokutana na wadau mbalimbali na wafanyabiashara wa mkoa wa Arusha akisema miongoni mwa dhamira zake ni kuifanya Arusha kuwa mikoa maarufu Kiuchumi na katika mpangilio mzuri kama yalivyo Majiji mengine makubwa duniani.
Makonda akitolea mfano wa kundi la vijana lililovuma kwa siku za karibuni mkoani hapa la "Wadudu", amesema haipendezi kuwa na Utambulisho wa aina hiyo ilihali mkoa wa Arusha umebarikiwa kuwa na vivutio vingi vya utalii na Ardhi inayokubali kilimo Maarufu cha Kahawa.
Aidha Paul Makonda ameonesha kusikitishwa na hali ya uchafu na wingi wa Mabango Katika Jiji la Arusha na kuagiza kuandaliwa kwa Mpango maalum utakaoweka Jiji katika mpangilio mzuri wenye kuzingatia matumizi ya Runinga za barabarani kwenye matangazo ya kibiashara badala ya kutumia mabango ya kubandika na kugongelea kwenye nguzo na kuta za nyumba za biashara zinazopatikana katikakati ya Jiji.
Katika kutekeleza maagizo ya Rais Samia Suluhu Hassan katika kuinua Utalii wa Arusha Mkuu huyo wa Mkoa ameendelea na vikao kazi mbalimbali vya kusikiliza na kutengeneza mazingira rafiki kwa wadau wa Utalii mkoani humo waweze kufanya shughuli zao kwa namna inayofaa na rafiki kwao.