Mambo 5 Ya Kufanya Kwenye Mtandao Kuwafikia Wateja Wengi na Kuuza Bidhaa Nyingi

  Рет қаралды 13,971

Dr. Said Said

Dr. Said Said

Күн бұрын

Jifunza kunasa wateja kama smaku hapa: goo.gl/SXFSzk
Kama wewe ni mjasiriamali mwenye bidhaa au huduma nzuri lakini unashindwa kuwafikia watu wengi kwenye mtandao basi hakikisha unanipa macho na masikio yako kwani huenda makala hii ikawa moja ya makala muhimu utakayosoma mwaka huu.
Kutokana na uzoefu wangu wa kutumia mtandao kupata wateja, nimegundua kuna mambo 5 ukiyafanya vizuri basi utawafikia watu wengi na kuuza bidhaa nyingi sana.
Mambo yenyewe ni:
1. Zingatia Ubora:
Ukiwa unatoa bidhaa au huduma nzuri kwenye soko yenye kutatua matatizo ya wateja wako, basi utapata majeshi ya watu watakaokusaidia kusambaza ujumbe kuhusu bidhaa yako bila ya wewe kuwalipa chochote.
Wajasiriamali wa Silicon Valley, Marekani wana msemo wao unaosema,
The goal is to develop a product so good that customers will move the products for us before we consider marketing it.
Yaani,
Lengo ni kutengeneza bidhaa nzuri sana kiasi ambacho wateja wetu watatutangazia kwenye soko kabla ya sisi kufikiria kuitangaza wenyewe.
Na moja kati ya sifa muhimu wawekezaji wa makumpuni ya Silicon Valley (akina Facebook) wanaangali ni bidhaa nzuri zinazoweza kutangazwa na watumiaji?
2. Kuwa Tofauti
Ukiwa tofauti unakumbukwa.
Moja ya kosa kubwa linalofanywa na wafanyabiashara wetu ni kuangalia washindani wako wanafanya nini na kuwaiga.
Ukifanya hivyo basi usitegemee biashara yako kudumu miaka mingi.
Kuwa mbunifu na jiweke tofauti kabisa na washindani wako.
Mfano mzuri ni kampuni ya viatu iitwayo Vibram Five fingers, viatu vilivyokaa kama glovu za mikono.
Walipoviingiza viatu vyao sokoni vilianza kuenea kama virusi vya flu na kila aliyekuwa anaviona viatu hivyo alikuwa akivitamani.
Kwa nini? Mbali na bidhaa yao kuwa nzuri, walikuwa tofauti kabisa na viatu vyengine.
Ukiwa tofauti utakumbukwa siku zote.
Hutafananishwa na mamia ya washindani wako wanaofanana.
Na kila ikiwa rahisi kukumbukwa inakuwa ni rahisi vile vile kuwafikia watu wengi.
3. Toa Kabla Hujapokea
Japokuwa umeanzisha biashara yako kutengeneza pesa, jiulize kitu gani unaweza kutoa BURE kabla ya kuuza bidhaa yoyote?
Hii ni muhimu sana kwani wateja wako watarajiwa hawakujui, hawakupendi na wala hawakuamini.
Kwa hivyo ukiwazawadia kitu chochote, utajenga uaminifu kwa urahisi na kwa kasi kubwa sana hususan katika mtandao.
Vitu unavyoweza kutoa ni kama:
- Ushauri
- Sampuli ya bidhaa
- Mafunzo (kama haya ninaokupa mimi)
- N.k. (Kuwa mbunifu)
Lengo la utoaji ni kuwaonesha wateja wako watarajiwa kuwa hupo pale kula pesa zao bali unawajali na unataka bidhaa / huduma unayotoa iwasaidie kutatua matatizo yao.
4. Tengeneza Smaku Ya Kunasa Wateja Kwenye Mtandao
Tengeneza mashine kwenye mtandao yenye kuwasiliana na wateja wako watarajiwa, kukujengea uaminifu na kukuuzia bidhaa zako kwa niaba yako.
Watu wengi nikiwaambia hili hawaamini kuwa ni jambo linalowezekana lakini kwa dunia ya sasa amini usiamini ni jambo ambalo mtu yoyote anaweza kufanya hata kama hana elimu ya kompyuta.
Hii ni topic ndefu kidogo ila kama unataka kujifunza zaidi nimetengeneza video yenye kueleza namna ya kufanya hivyo hapa.
5. Tangaza! Tangaza! Tangaza!
Na jambo la tano na la muhimu sana la kufanya kuweza kuwafikia watu na kuuza bidhaa nyingi ni kutangaza.
Matangazo ni kama petroli kwenye gari lako.
Ukiacha kutangaza biashara yako haisogei mbele. Inakwama au inarudi nyuma.
Kwa vile washindani wamekuwa wengi kutangaza si jambo la hiari.
Ila ni muhimu kuzingatia matunda unayopata kutokana na kila tangazo uweze kuboresha na yazidi kukuletea faida.
Lengo ni kuwekeza pesa yenye kukusaidia kuleta mauzo yenye faida kubwa kuliko gharama za matangazo yako na kuendelea kufanya hivyo kila siku ili biashara yako ikuwe.
Ukiwa na mfumo mzuri kwenye biashara yako (ya mtandaoni na nje ya mtandao) kazi yako kubwa itakuwa ni
Kutangaza na
Kuboresha bidhaa na huduma zako
Kama una mchango au swali lolote, comment hapo chini.
Wako,
Dr. Said Said - CEO Online Profits
• Mambo 5 Ya Kufanya Kwe...

Пікірлер: 34
@mahmoudmzee-pr3vs
@mahmoudmzee-pr3vs Жыл бұрын
Shukran for good guidelines
@onesmolaurent210
@onesmolaurent210 Жыл бұрын
Kiongozi nashukuru sana kwa somo lako zuri sana , lakini mimi bilingual kwenye biashara ya suppliant nashindwa kupata wateja sijjajua Jinsi ya kujibrand
@user-vn5xu8sm4g
@user-vn5xu8sm4g Жыл бұрын
Kaka hongeraa asante asante sana🙏🙏
@dr.saidsaid
@dr.saidsaid Жыл бұрын
Asante
@avand4237
@avand4237 Жыл бұрын
Nilichelewa sana kuonana na Dr Said said popote ulipo Mungu akubaliki sana.
@josephmwinulla3737
@josephmwinulla3737 Жыл бұрын
Mafundisho ni mazuri sana. So resourceful and educative. Thank you.
@khadijamwinyi5873
@khadijamwinyi5873 2 жыл бұрын
Shukrni Sana umeeleweka vizuri umenisaidia pakubwa Dr
@godlovebruno3395
@godlovebruno3395 6 жыл бұрын
Ahsante kwa kutufumbua macho
@zuberyhaule5732
@zuberyhaule5732 4 жыл бұрын
Shukrani
@khadijamwinyi5873
@khadijamwinyi5873 2 жыл бұрын
Dr Mimi nafanya biaahara ya Network market ya Foreverliving product naipenda Sana natumia njia ya kuongea nawatu Ana kwa Ana na mikutano midogomidogo Ila bado cijawa nawateja wengi naomba msaada
@mahadimatsawily5809
@mahadimatsawily5809 3 жыл бұрын
Ahsante
@zainabushabani3881
@zainabushabani3881 5 жыл бұрын
Samahani naomba namba yako
@jameseligius9459
@jameseligius9459 7 жыл бұрын
awesome
@vailethjohn4067
@vailethjohn4067 4 жыл бұрын
Kwajina naitwa vailet mjasiliamari mdogo, nauza mchele lakini napata wakati mgum kupata wateja, mpaka nakata Tama naomba msahada wakuelimishwa, Asante
@dr.saidsaid
@dr.saidsaid 4 жыл бұрын
Vaileth John huo mchele ni brand yako au brand ya kampuni nyengine?
@annetcliford8801
@annetcliford8801 Жыл бұрын
Nimechelewa kujua ila umenifundisha kitu nataka kuazisha biashara ya chakula Ila kwa kupikia nymbni alafu nisambaze nitapata je wateja naomba wsp namba yko iliunileweshe nitapataje wateja online
@silverfinancialservicescol9306
@silverfinancialservicescol9306 6 жыл бұрын
Dr. Habari asante kwa somo nataka kujua nalipiaje tangazo ninapotaka kutumia social network haya ya fb nalipia kupitia vp
@INTERPRENUER42
@INTERPRENUER42 2 жыл бұрын
🔥🔥
@mickidadyplanet6476
@mickidadyplanet6476 4 жыл бұрын
Sante sana...naomba kujua unaweza kufanya matangazo kwa kutumia smart phone au mpaka computer???
@sylveresentore8726
@sylveresentore8726 3 жыл бұрын
Kwangu Mimi nitawezaj kujenga vyashara nikiwa nauza asali
@conniesilayo250
@conniesilayo250 5 жыл бұрын
Kaka unaongea kitu chenye ukweli.
@richkinji2583
@richkinji2583 2 жыл бұрын
Hutoi number bro
@taqiyaommy5470
@taqiyaommy5470 4 жыл бұрын
Nomba namba yako
@dr.saidsaid
@dr.saidsaid 4 жыл бұрын
Taqiya Ommy tupigie hapa 0679 536927
@MwamvuaSihaba-hf2kw
@MwamvuaSihaba-hf2kw Жыл бұрын
Kwaiyo kama unataka kutuma matangazo mtandaoni iyo dollar 5 unaweka mb au vipi hapa sijafahamu
@dr.saidsaid
@dr.saidsaid Жыл бұрын
Unawalipa Facebook/Instagram
@sarahkyando189
@sarahkyando189 6 жыл бұрын
naomba msaada wanamba whatsap
@mashakaabduly4506
@mashakaabduly4506 6 жыл бұрын
So great
@leocadiahussein6744
@leocadiahussein6744 4 жыл бұрын
Naomba uniunge kwa group lako wsp namba 0683052634
@dr.saidsaid
@dr.saidsaid 4 жыл бұрын
Wasiliana nasi hapa 0679 536927
Magic or …? 😱 reveal video on profile 🫢
00:14
Andrey Grechka
Рет қаралды 68 МЛН
Новый уровень твоей сосиски
00:33
Кушать Хочу
Рет қаралды 2,6 МЛН
How to win a argument
9:28
ajaxkmr
Рет қаралды 526 М.
Ufanye nini watu wa kupende zaidi?
9:09
Joel Nanauka
Рет қаралды 131 М.
Njia Ya Bora Ya Kuuza Bidhaa Kwa Wingi - Joel Nanauka
6:09
Joel Nanauka
Рет қаралды 23 М.
Jinsi ya Kuingiza Hadi Milioni 100 Kwa Mwaka Katika Biashara Yako
26:34
Njia 4 Kubwa Unazoweza Kutumia Kumshawishi Mteja.
7:01
Joel Nanauka
Рет қаралды 102 М.
Jinsi ya Kuuza Bidhaa za Bei za Juu Sana Kwa Urahisi
11:33
Dr. Said Said
Рет қаралды 7 М.
Magic or …? 😱 reveal video on profile 🫢
00:14
Andrey Grechka
Рет қаралды 68 МЛН