Рет қаралды 1,506
Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi, Godfrey Kasekenya amemtaka mkandarasi M/S SINOHYDRO COOPERATION LIMITED anayejenga miundombinu ya mfumo wa usafiri wa mabasi yaendayo haraka BRT 3, KM 23.3 kuanzia katikati ya jiji la Dar es salaam hadi Gongolamboto kuhakikisha ujenzi huo unajengwa kwa viwango vya kimataifa kutokana na umuhimu wa barabara hiyo.
Akikagua ujenzi wa barabara za mabasi yaendayo kwa haraka tarehe 6 Agosti 2024, Naibu Waziri Kasekenya amesema barabara hiyo ni lango la jiji la Dar es salaam na taifa kwa ujumla hivyo Serikali inategemea kuwa itakuwa barabara ya mfano kwa ubora na muonekano.
#wizarayaujenzi