Рет қаралды 417
Kujenga utajiri ni kazi iliyokamilika, ambayo mtu anapaswa kuifanya kwa uhakika. Ili mtu kufanikisha hilo, mtu anapaswa kuwekeza muda, nguvu na fedha.
Watu wengi huwa wanadhani utajiri unatokea tu pale wanapokuwa na kipato kikubwa. Lakini ukweli ni kwamba kipato kikubwa siyo utajiri. Maana mara nyingi kipato kikubwa huwa kinaambatana na matumizi makubwa.
Karibu kwenye kipindi hiki ujifunze jinsi unavyopaswa kuwekeza muda, nguvu na fedha kujenga utajiri mkubwa kwenye maisha yako.