Рет қаралды 1,309
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj. Dk. Hussein Ali Mwinyi amehimiza Wananchi na Waumini wa dini ya Kiislamu nchini umuhimu wa kuendelea kuiombea amani Zanzibar na viongozi wake, hususan kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi wa 2025 ambapo amesema kunaanza kuonekana viashiria vingi vya uvunjifu wa amani.
Amesema ni vema kumrudia Mungu na kuendelea kuiombea nchi yetu ili iendelee kuwa na amani kwani maendeleo hayatakuja bila amani.
Alhaj Dk.Mwinyi ameyaeleza hayo wakati akitoa salamu baada ya Sala ya Ijumaa katika Msikiti wa Rahman, Meli Nne, Taveta, Wilaya ya Magharibi B, Unguja, Alhaj Dk. Mwinyi amesema ili muumini wa dini ya Kiislamu afanikiwe, ni lazima awe na imani na aifuatishe kwa matendo mema; vyote viende sambamba ili kufanikisha kwani kufanya matendo bila imani si sawa na kufanya vyote kwa wakati mmoja ili kupata radhi za Mwenyezi Mungu.
Rais Dk.Mwinyi akiwa na viongozi mbalimbali wa Serikali na dini waliungana na waumini hao wa Melinne Taveta.
Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi na Utawala Bora Mwalimu Haroun Ali Suleiman amesema mawazo na mipango aliyokua nayo Rais Dk.Mwinyi wananchi wakiendelea kumuunga mkono nchi itapiga hatua zaidi kwa muda mchache.
Nae Katibu Mtendaji wa Ofisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khalid Ali Mfaume amemuelezea Alhaj Dk.Mwinyi kuwa ni kiongozi ambae moyo wake ni mkunjufu hivyo amewataka waumini hao kusimama pamoja na kumuombea dua.
Waumini wa Msikiti huo nao wamempongeza Rais Mwinyi kwa jinsi anavyojitolea kwa kutengeneza yale yote aliyowaahidi wananchi wakati wa alipoomba kura kwa wananchi.
Zanzibar
▪️RAIS MWINYI AHIMIZA AMANI NA UTULIVU
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi amewahimiza waumini wa Dini ya Kiislamu kuendelea kuiombea nchi dua na viongozi wake waendelee kudumisha amani, mshikamano utulivu kuelekea uchaguzi mkuu mwakani.
Dkt.Mwinyi aliyasema hayo alipojumuika na Waumini wa Dini ya Kiislamu katika Sala ya Ijumaa Msikiti wa Rahman Taveta, Mkoa wa Mjini Magharibi tarehe 2 Agosti 2024.
Aidha Rais Dkt.Mwinyi amesema hakuna maendeleo pasipokuwepo amani na utulivu.