SHIMO NYUMBA YA UHARIBIFU ( DAY ONE) - PASTOR SUNBELLA KYANDO

  Рет қаралды 19,696

Reality of Christ Church

Reality of Christ Church

2 жыл бұрын

Mithali 15:11
[11]Kuzimu na Uharibifu vi wazi mbele za BWANA;
Si zaidi basi, mioyo ya wanadamu?
Kuzimu ni eneo ambalo lipo katika ulimwengu wa roho,kwa maana hiyo hata uharibifu pia ni eneo ambalo lipo katika ulimwengu wa roho,na hadi Neno la Mungu linasema kuwa "vi wazi mbele za Bwana" inamaanisha kuwa ni maeneo ambayo kwa macho ya nyama hayaonekaniki.
Neno la Mungu linaendelea kuelezea kuhusu huu uharibifu katika kitabu cha Ayubu;
Ayubu 26:6
[6]Kaburi li wazi mbele yake,
Uharibifu nao hauna kifuniko.
Tofauti ya kaburi na uharibifu ni kuwa kaburi baada ya kuzikiwa hufunikwa lakini uharibifu hauna kifuniko,kwa maana nyingine; kama kaburi ni shimo hata uharibifu nao pia ni shimo kasoro tu halina kifuniko,yaani halifunikwi.Ni sawa chupa ya chai,ukimmiminia mtu mmoja ukimaliza utaifunika lakini kama kuna foleni ya watu wa kuwamiminia kwenye vikombe hautoifunika hadi uwamalize.Kwa maana hiyo uharibifu ni shimo ambalo lipo busy sana,watu wanawekwa hapo sana.Kumbuka UHARIBIFU SIO MATOKEO BALI NI ENEO(LOCATION).
Na hili jambo lilimtokea pia Daudi;
Zaburi 40:1-2
[1]Nalimngoja BWANA kwa saburi,
Akaniinamia akakisikia kilio changu.
[2]Akanipandisha toka shimo la uharibifu,
Toka udongo wa utelezi;
Akaisimamisha miguu yangu mwambani,
Akaziimarisha hatua zangu.
Mungu baada ya kusikia kilio cha Daudi kitu cha kwanza alichofanya ni kumuhamisha eneo(location) alimokuwemo,yaani shimo la uharibifu.Yeyote anayekuwa ndani ya shimo hakuna kitu atakachokifanya na kikaenda kwa sababu yupo shimoni.Kuna watu kimwili wapo maofisini lakini kiroho wamewekwa kwenye shimo la uharibifu, mshahara wanapata lakini hakuna matunda anayokula kutokana na kazi yake.
Biblia inaendelea kusema kuwa "...toka udongo wa utelezi".
Kwa maana nyingine hata mtu huyu akijitahidi kutoka kwenye shimo bado atateleza na kuanguka tena,na mara nyingi huumia.Ndio maana kila ambavyo unajitahidi kupiga hatua ndivyo ambavyo unakutana na vitu vya kukuumiza sana na unajikuta unarudi nyuma.
Kwa Daudi ilibidi Mungu aingilie kati na kumtoa kwenye hilo shimo, katika sehemu inayofuata tutakuwa na MAOMBEZI na kila shimo la uharibifu ulilowekwa Mungu ataenda kukutoa.
UNAWEZA WASILIANA NASI AU KUTUMA SADAKA YAKO KWA NAMBA HII : 0657 173 322
Unaweza kutufuatilia katika mitandao yetu ya kijamii
Like our Facebook: / therealityof. .
Follow our Instagram: / realityofch. .
Subscribe our KZbin: kzbin.info/door/67L...
Also Subscribe Roc worshippers youtube channel: / @rocworshipperz
and Subscribe Pastor Sunbella Kyando KZbin
/ @pastorsunbellakyando

Пікірлер: 41
@leonardsr8994
@leonardsr8994 2 жыл бұрын
Jana wakati somo hili linafundishwa ndio ilikua siku ya kwanza kufika Reality Of Christ. Nilipoingia tu moyo wangu ulitulia tuliiiiiiiiiiiii. Asante Roho Mtakatifu kwa hii madhabahu
@petermunuo1657
@petermunuo1657 Жыл бұрын
Amen mtumishi barikiwa sana
@angeljoseph4666
@angeljoseph4666 Жыл бұрын
Amen
@Magrethmvwango-bi9gw
@Magrethmvwango-bi9gw Жыл бұрын
Amen 🙏 mungu naomba simama pamoja Nami mungu naomba nitetee wote wanao pigana Nami mungu naomba shughulika nao🙏Amen
@danstonecool1734
@danstonecool1734 2 жыл бұрын
amen
@loveandnature2821
@loveandnature2821 2 жыл бұрын
ASANTE YESU KRISTO MUNGU WA SUNBELLA KYANDO. NAPOKEA USHUHUDA. HALLELUJAH
@joycekariuki46
@joycekariuki46 2 жыл бұрын
Mtumishi umenifundisha Sana haswa katika angaa ya kiroho roho natoka kenya 🇰🇪 kumbe watoto wa giza ni werevu hivyo but pia sisi tukisha jua principles za kiroho tutawashinda ndani Christu aliye mkombozi wetu
@paulashuma3042
@paulashuma3042 2 жыл бұрын
Amen🙏nilikuwa nasubiri iwe downloaded sana,Asante Yesu Kristo kwa kufanikisha hili.nahamu sana siku nikanyage madhabahu hii tena nilikanyaga miaka mingi sana jumamosi moja..maana kwa kuangalia tuu napokea napokea.nampenda huyu Pastor .such a great Men of God🙏
@Miriam84Akizimana
@Miriam84Akizimana 2 жыл бұрын
This man of God is sent by God to our nation 🙏❤️🙏 I love him , he is a father 🙏
@paulchristian5071
@paulchristian5071 Жыл бұрын
Najifunza saana kwako MTU WA MUNGU.
@kilangoester3112
@kilangoester3112 2 жыл бұрын
Shalom! Nimepata ufahamu.Nahitaji maombi zaidi.
@catherinewanjiku2655
@catherinewanjiku2655 2 жыл бұрын
AMEN AMEEN AMEEN AMEEN
@lucimueni9746
@lucimueni9746 2 жыл бұрын
Hallelujah Niko Kenya ninaweza aje kuwasiliana na wewe mtumishi wa Mungu....kwa kweli ukona talanta ya kuhubiri injili
@jeanbaptiste5512
@jeanbaptiste5512 2 жыл бұрын
❤️❤️❤️ Mchungaji usikose kuniombea napenda kushirikiana nanyi hadi tamati live lakini kazi ninayofanya hainiruhusu.
@shamimushittindi1418
@shamimushittindi1418 2 жыл бұрын
My fav pastor
@annstersianganga6772
@annstersianganga6772 2 жыл бұрын
Thank you JESUS
@najimaharrison8543
@najimaharrison8543 2 жыл бұрын
Amen nimefungulika katika jina la YESU
@lizzymachocho2948
@lizzymachocho2948 2 жыл бұрын
Asante mtumishi kwa hili somo,wakati nilipofunga na kumuombea mtoto wangu nilipata ndoto kwamba yupo ndani ya shimo,nikamuita akatokea na nikampandisha,alikua amevaa nguo nyeupe hadi viatu,sasa nimeelewa.ubarikiwe sana sanaaaaa
@sifasylvie3941
@sifasylvie3941 2 жыл бұрын
amen asante sana kwa mafundisho iyi tunaendelea ku tiwa nguvu ,na nina amini roho wa mungu ataenda kufungua maisha yangu,na kusihi baba mchungaji nami uniombee ili niweze kutoka ndani ya gereza la shetani naamini mungu atasema na wewe kwaajili yangu.asante.
@victoremmanuelmwasalwiba9926
@victoremmanuelmwasalwiba9926 2 жыл бұрын
Amen 🙏
@saramtei4371
@saramtei4371 2 жыл бұрын
Amen dada hakika nimetoka kwenye shimo nakupend babaang kwa jins mungu anavyokutumia hakika natoka mahal nakwenda mahal
@tupokengwala2027
@tupokengwala2027 2 жыл бұрын
Amen! Asante Yesu
@veronikaaugustino2258
@veronikaaugustino2258 2 жыл бұрын
AMINA Naamin kileMUNGU anataka kufanya kupitia hili NENO Nimekipokea tayar AMINA
@ernetaissaaluta3185
@ernetaissaaluta3185 2 жыл бұрын
Amen ubarikiwe sana pastor
@angeljoseph4666
@angeljoseph4666 2 жыл бұрын
Asante Mungu amen 🙏🙏🙏
@ruthjoel2426
@ruthjoel2426 2 жыл бұрын
Amen 🙏🙏🙏🙏
@mhamdahmd7758
@mhamdahmd7758 2 жыл бұрын
Amen Amen Mungu ..unikumbuke
@neemasindwa6925
@neemasindwa6925 2 жыл бұрын
Amen ubarkiwe sana umenifungua
@bennamuchau6487
@bennamuchau6487 2 жыл бұрын
Damu ya Yesu!
@emmymatigula4870
@emmymatigula4870 2 жыл бұрын
Mpakwa mafuta Huku niliko niombee Nitakupata vipi? Kilichotokea kwangu kimefunuliwa ktk hili somo Laa!wakati wa kupona ni huu Huyu MUNGU BABA ALIYEHAI Azidi kukufunulia tupone na tuwe washindi ndani ya YESU ALIYEHAI Amina .
@judithngasa1370
@judithngasa1370 2 жыл бұрын
Ameeen
@addo2014
@addo2014 2 жыл бұрын
Ooh Mungu ili neno umelileta kwaajili ya maisha yang ❤🙏
@annabaramay3793
@annabaramay3793 2 жыл бұрын
Nimetoka shimoni kwenye uharibifu wa Kila aina
@angeange4342
@angeange4342 2 жыл бұрын
Asante kamafundisho
@lindajohn1558
@lindajohn1558 2 жыл бұрын
Kweli mtumishi ubarikiwee unatufungua wengi katika ulimwengu wa Roho
@angeange4342
@angeange4342 2 жыл бұрын
@@lindajohn1558 mimisio mutumishi miminimlika
@carolinamponji4294
@carolinamponji4294 2 жыл бұрын
Mungu wa madhabahu hii ni wamoto ananisaidia sana
@angeange4342
@angeange4342 2 жыл бұрын
@@carolinamponji4294 nikweli kabsa
@annabaramay3793
@annabaramay3793 2 жыл бұрын
Nimeelewa SoMo kuanzia leo nimetoka kwenye shimo la uharibifu kwa jina la Yesu
@heriethkitururu4401
@heriethkitururu4401 2 жыл бұрын
Mungu asante kwa mafundisho aya
@rosanoella5715
@rosanoella5715 2 жыл бұрын
Mungu awabariki sana
JE MTU ALIYEOKOKA ANAHITAJI KUFUNGULIWA? BY PASTOR SUNBELLA KYANDO
1:00:49
Reality of Christ Church
Рет қаралды 16 М.
What it feels like cleaning up after a toddler.
00:40
Daniel LaBelle
Рет қаралды 84 МЛН
Best KFC Homemade For My Son #cooking #shorts
00:58
BANKII
Рет қаралды 67 МЛН
КАК ДУМАЕТЕ КТО ВЫЙГРАЕТ😂
00:29
МЯТНАЯ ФАНТА
Рет қаралды 10 МЛН
TAMBUA MLANGO USIOFUNGULIWA NA MUNGU - Min. Sunbella Kyando
1:08:00
Reality of Christ Church
Рет қаралды 33 М.
3. KUONDOA MAZUIO KATIKA MIFUMO YANAYOZUIA  KUFANIKIWA KWAKO || MWL CHRISTOPHER MWAKASEGE || Singida
3:17:18
CHRISTOPHER AND DIANA MWAKASEGE CHANNEL
Рет қаралды 27 М.
SADAKA NA FUNGU LA KUMI
48:56
RGC-TOANGOMA
Рет қаралды 19 М.
MAOMBI YA FAMILIA   DODOMA - PASTOR SUNBELLA KYANDO
1:06:00
Reality of Christ Church
Рет қаралды 11 М.
KKKT USHARIKA WA KIJITONYAMA : IBADA YA EVENING GLORY  20/07/2022
1:32:30
KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH
Рет қаралды 10 М.
FAIDA ZA KUMTUMIKIA MUNGU #Bishop_Dr_Josephat_Gwajima_LIVE:  #Sunday_23Sept2018 #UbungoTZ
2:46:25
Uelewe ulimwengu wa Roho Ufanikiwe katika Maisha II
32:15
Reality of Christ Church
Рет қаралды 18 М.
4. KUONDOA MAZUIO KATIKA MIFUMO YANAYOZUIA  KUFANIKIWA KWAKO || MWL CHRISTOPHER MWAKASEGE || Singida
3:27:53
CHRISTOPHER AND DIANA MWAKASEGE CHANNEL
Рет қаралды 23 М.
ROHO MTAKATIFU NA NGUVU ZAKE - Pastor Sunbella Kyando
1:30:43
Reality of Christ Church
Рет қаралды 29 М.
What it feels like cleaning up after a toddler.
00:40
Daniel LaBelle
Рет қаралды 84 МЛН