Рет қаралды 552
Nyota ya uongozi ya Shujaa huyu ilianza kung'aa pale alipoanza kujihusisha na masuala ya kisiasa licha ya kuwa Mtumishi wa Serikali.
Lawi Nangwanda Sijaona alijiunga na Chama cha Tanganyika African Association(TAA), huku akifanya shughuli hizo za kisiasa kwa usiri mkubwa.
Wakati harakati za kutafuta Uhuru zikiendelea, aliwahi kumkaribisha nyumbani kwake Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambapo walipanga mikakati mbalimbali iliyowezesha kupatikana kwa Uhuru
Shujaa huyu pia alishiriki katika kuanzishwa kwa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na baadae JKT ilimpatia Tuzo kama kumbukumbu ya kutambua mchango na fikra zake zilizowezesha kuanzishwa kwa Jeshi hilo mwaka 1963.
Mbali na harakati hizo za kupigania Uhuru, Lawi Nangwanda Sijaona pia anakumbukwa na wapenzi wa soka nchini hasa wa Klabu ya Yanga ya jijini Dar es Salaam, kwani alikuwa mmoja wa watu waliotoa mchango mkubwa katika kuhakikisha jengo la klabu hiyo linajengwa mitaa ya Twiga na Jangwani, Dar es Salaam..