Рет қаралды 120,867
Timu ya taifa ya wanawake ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Queens, imetinga fainali ya Kombe la CECAFA baada ya kuwaondosha Uganda kwa bao 1-0 kwenye nusu fainali kali iliyofanyika jioni ya leo dimbani Azam Complex Chamazi.
Mchezo huo ulioshuhudia kipindi cha kwanza kikimalizika kwa suluhu, uliamuliwa kwa goli la kipindi cha pili la mkongwe Asha Rashid maarufu kama Asha Mwalala.