Рет қаралды 18
Wakazi wa kata ya Kasoli na maeneo jirani wameondokana na changamoto ya kivuko katika mto Nyamilungu baada ya diwani wa kata hiyo kwa kushirikiana na wananchi pamoja na wadau wengine kufanikisha ujenzi wa kivuko katika mto huo.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kivuko hicho diwani wa kata ya Kasoli ambaye pia ni mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Bariadi Lucas Mayala amesema ameamua kufanya ujenzi wa kivuko hicho kutokana na maombi ya wakazi wa eneo hilo aliyoyapata wakati wa ziara yake ya kusikiliza kero za wananchi.
MWISHO.